Friday, November 28, 2014

MOYES AMTEUA MCKINLAY KUWA MSAIDIZI WAKE REAL SOCIEDAD.

MENEJA wa klabu ya Real Sociedad, David Moyes amemteua Billy McKinlay kuwa msaidizi wake. Mckinlay ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Scotland amekuwa hana kibarua toka atimuliwe na klabu ya Watford baada ya kusimamia mechi mbili pekee. Moyes sasa ameamua kumchukua Mckinlay amsaidie katika benchi lake la ufundi baada ya kuiongoza Sociedad kupata sare ya bila kufungana katika mechi yake ya kwanza dhidi ya Deportivo La Coruna. Ijumaa hii Moyes anakabiliwa na kibarua kingine pale Sociedad itakapoikaribisha Elche katika mchezo wake wa kwanza akiwa katika uwanja wa nyumbani.

No comments:

Post a Comment