Friday, November 28, 2014

SIDHANI KAMA ARSENAL WANANIHITAJI TENA - KLOPP.

MENEJA wa klabu ya Brussia Dortmund, Jurgen Klopp ametania kuwa mashabiki wa Arsenal hawatamuhitaji tena baada ya kuona timu yake ikitandikwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya juzi. Klopp amekuwa akihusishwa na tetesi za kuchukua mikoba ya kionoa Arsenal katika wiki kadhaa zilizopita baada ya kuzuka msukumo kwa Arsene Wenger kufuatia kuanza vibaya msimu wa Ligi Kuu. Kocha huyo amekiri hivi karibuni kuwa anadhani anaweza kumudu kuhamia katika Ligi Kuu kama akiamua kuondoka Dortmund lakini sasa anadhani nafasi yake ya kutua Arsenal imetoweka. Akihojiwa Klopp amesema hafikirii baada ya kiwango cha Dortmund walichokionyesha katika Uwanja wa Emirates kama mashabiki wa Arsenal watamuhitaji. Klopp aliteuliwa kuwa kocha wa Dortmund kuanzia mwaka 2008 na kuisaidia timu hiyo kushinda mataji mawili ya Bundesliga, Kombe la Ujerumani, Supercup na kutinga fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment