Thursday, November 27, 2014

VERMAELEN KUKAA NJE YA UWANJA MIEZI MITANO.

BEKI wa Barcelona, Thomas Vermaelen anatarajiwa kufanyiwa upasuaji ili kurekebisha tatizo la paja linalomsumbua wiki ijayo na anategemewa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi minne mpaka mitano. Beki huyo wa kati wa kimataifa wa Ubelgiji ambaye alipata majeruhi hayo wakati akiitumikia nchi yake katika mchezo dhidi ya Urusi katika Kombe la Dunia Juni mwaka huu mpaka hajacheza mechi yeyote ya mashindani toka ajiunge na timu hiyo akitokea Arsenal Agosti. Usajili huo umekuwa jambo lililoifedhehesha bodi ya klabu hiyo. Vermaelen mwenye umri wa miaka 29 amekuwa akisummbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara toka alipokuwa Arsenal ambapo amecheza mechi 21 pekee msimu uliopita akiwa na washika bunduki hao wa London.

No comments:

Post a Comment