Thursday, November 27, 2014

HALI YA PELE YAENDELEA KUIMARIKA.

AFYA ya nguli wa soka wa Brazil, Pele inaendelea kuimarika lakini bado ameendelea kuwa chini ya uangalizi maalumu katika hospitali jijini Sao Paulo ambako alilazwa siku tatu zilizopita kutokana na kupata maambukizi katika njia ya mkojo. Katika taarifa iliyotolewa na hospitali hiyo ya Albert Einstein imedai kuwa hali ya nguli huyo inaendelea kuimarika pamoja na kuwa bado amewekwa katika wodi ya wagonjwa mahututi. Mapema baada ya kuthibitika kuwa Pele alipelekwa hospitali Jumatatu iliyopita, hospitali hiyo ilidai kuwa vipimo alivyofanyiwa vimeonyesha kuwa alipata maambukizi katika njia ya mkojo. Wakala wake Jose Fornos alidai kuwa mteja wake alichoka baada ya kupokea wageni wengi na kuongeza kuwa Pele anaweza kupokea matibabu yanayoweza kuchukua zaidi ya miezi mitatu. Pele alifanyiwa upasuaji kuondoa mawe katika figo Novemba 13 mwaka huu na alionekana kuwa katika hali nzuri aliporuhusiwa siku mbili baadae kwa kufungua dirisha lake na kuwapungia mkono mashabiki ambao walikusanyika hospitali.

No comments:

Post a Comment