Thursday, November 27, 2014

EVERTON, SPURS ZUFUZU EUROPA LEAGUE.

KLABU za Ligi Kuu nchini Uingereza Everton na Tottenham Hotspurs zimefanikiwa kufuzu hatua ya mtoano ya michuano ya Europa League jana huku Celtic nao wakifuata nyayo hizo pamoja na kufungwa na Salzburg nyumbani. Everton wao walisonga mbele katika hatua ya timu 32 bora wakiwa kama vinara wa kundi H baada ya kuitandika mabao 2-0 VfL Wolfsburg katika mchezo uliochezwa nchini Ujerumani. Tottenham wao walisonga mbele katika kundi C kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 nyumbani kwa vinara wa Ligi Kuu ya Israel Partizan Belgrade huku Celtic wao pamoja na kufungwa mabao 3-1 na Salzburg jijini Glascow lakini wanasonga mbele huku wakiwa wamebakiwa na mchezo mmoja mkononi. Timu zingine zilizofuzu jana ni Dinamo Moscow ambao waliwatandika Panathinaikos kwa mabao 2-1 na kujihakikishia nafasi yao katika kundi E huku Inter Milan nao wakisonga mbele katika kundi F kwa kuifunga Dnipro kwa mabao 2-1 katika Uwanja wa san Siro. Wengine ni Napoli ambao sare ya bila ya kufungana dhidi ya Sparta Prague katika kundi I ilitosha kuwavusha huku Fayenoord, Dynamo Kiev na Trabzonspor nazo zikifuzu baada ya kushinda michezo yao.

No comments:

Post a Comment