Thursday, November 27, 2014

MMILIKI WA WIGAN MATATANI KWA KUKASHIFU.

MMILIKI wa klabu ya Wigan Athletic, Dave Whelan ameshitakiwa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa kuwatukana watu wenye asili ya Kiyahudi na Kichina wakati akifanya mahojiano na gazeti. Katika taarifa yake FA inatuhumu Whelan kwa kufunja sheria za chama hizo kwa kutoa kauli hiyo kuudhi. FA iliendelea kudai kuwa inampa Whelan mpaka Desemba 5 kuwa amejibu tuhuma hizo kabla ya hatua zaidi hazijaendelea kuchukuliwa. Katika mahojiano yake na gazeti la Guardian baada ya kumtangaza kocha mpya Malky Mackay Whelan alikaririwa akidai kuwa watu kutoka China wana upeo mdogo huku akiwaambia Wayahudi kuwa wanapenda hela. Kiongozi wa jamii wa Wachina Jenny Wong alilaani vikali kauli hiyo ya Whelan huku kiongozi wa jamii ya Kiyahudi naye akidai kuwa kuomba radhi pekee kutokana na kauli yake hiyo haitoshi.

No comments:

Post a Comment