Friday, November 28, 2014

RODRIGUEZ, DI MARIA, SCHWEINSTEIGER WAONGOZA ORODHA YA VIUNGO WATEULE KATIKA KIKOSI CHA FIFPro WORLD XI 2014.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limetoa orodha ya wachezaji nafasi ya kati 15 ambao watapigiwa kura kwa ajili ya uchaguzi wa kikosi cha dunia ambapo majina matatu pekee ndio yatashinda nafasi hiyo. Kikosi hicho kinachojulikana kama World XI 2014, ambacho huteuliwa kwa kura za wachezaji duniani kote kinatarajiwa kutangazwa rasmi katika sherehe za utoaji tuzo ya Ballon d’Or Januari 12 mwakani. Wote waliojumuishwa katika orodha hiyo ni nyota waliokuwemo katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Brazil akiwemo mfungaji bora James Rodriquez wa Colombia pamoja na Angel Di Maria ambaye timu yake ya Argentina ilishika nafasi ya pili pamoja na Bastian Schweinsteiger anaewawakilisha mabingwa wa dunia Ujerumani. Cristiano Ronaldo na Lionel Messi wao wanatarajiwa kuwemo katika orodha ya washambuliaji ambayo itatolewa Desemba mosi mwaka huu, wakati wateule wa nafasi ya golikipa na mabeki wao wakiwa tayari wameshatangazwa. Orodha kamili ya wachezaji hao na timu zao ni pamoja na Xabi Alonso (Bayern Munich), Angel Di Maria (Manchester United), Cesc Fabregas (Chelsea), Eden Hazard (Chelsea), Xavi (Barcelona), Andres Iniesta (Barcelona), Toni Kroos (Real Madrid), Luka Modric (Real Madrid), Mesut Ozil (Arsenal), Andrea Pirlo (IJuventus), Paul Pogba (Juventus), James Rodriguez (Real Madrid), Bastian Schweinsteiger (Bayern Munich), Yaya Toure (Manchester City), Arturo Vidal (Juventus)

No comments:

Post a Comment