Monday, December 1, 2014

ORODHA YA WATAKAOGOMBEA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA AFRIKA HADHARANI.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limetangaza orodha ya wachezaji watano watakaogombea tuzo ya mchezaji ya mchezaji bora wa mwaka wa Afrika. Kabla ya kufanya mchujo CAf ilitoa majina majina ya wachezaji ya wachezaji 25 wa Afrika wanaocheza ligi mbalimbali duniani kote. Watano waliopenya ni pamoja na Vincent Enyeama na Ahmed Musa wa Nigeria, Asamoah Gyan wa Ghana, Pierre-Emerick Aubemeyang wa Gabon na na nyota nayeshikilia tuzo hiyo kwasasa Yaya Toure kutoka Iviry Coast. Majina hayo yatachujwa tena na kubakia matatu kabla ya sherehe za utoaji tuzo za CAF zitakazofanyika jijini Lagos Januari 8 mwaka huu. Mbali na orodha hiyo CAF pia iliteua orodha ya wachezaji watano ambao wanasakata kabumbu ndani ya bara la Afrika watakaogombea tuzo hiyo.

No comments:

Post a Comment