Monday, December 29, 2014

AFCON 2015: LEMINA AICHOMOLEA GABON.

MCHEZAJI nyota Mario Lemina ambaye alikuwemo katika kikosi cha vijana chini ya miaka 20 cha Ufaransa kilichonyakuwa Kombe la Dunia mwaka jana amekataa mwaliko wa kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Gabon kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon. Kocha wa Gabon Jorge Costa itabidi aende katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Januari 17 mpaka Februari 8 bila kiungo huyo wa Marseille. Lamina ambaye ni mzaliwa wa Gabon aliandika katika mtandao wake wa kijamii wa twitter kuwa yote yanayosemwa ni tetesi lakini tayari alifanya mawasiliano na nchi hiyo kuwa hatakwenda katika michuano hiyo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 ana matumaini ya kuitwa katika kikosi cha timu ya wakubwa ya Ufaransa. Mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubemeyang ni mojawapo ya jina kubwa lililomo katika kikosi cha Gabon ambacho pia kinawajumuisha beki wa Cardiff City Bruno Ecuele Manga na mshambuliaji wa Charlton Frederick Bulot. Gabon wamepangwa katika kundi A sambamba na wenyeji Guinea ya Ikweta, Burkina faso na Congo Brazzaville.

No comments:

Post a Comment