Monday, December 29, 2014

AFCON 2015: MALI YATAJA SILAHA ZAKE.

MODIBO Maiga ametajwa katika kikosi cha wachezaji 23 cha timu ya taifa ya Mali kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon huko Guinea ya Ikweta pamoja na kukosa mechi zote za kufuzu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Metz ya Ufaransa akitokea West Ham United hajaitumikia nchi yake kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja. Mfungaji kinara wa timu ya Wolverhampton Wanderers Bakary Sako ambaye amefunga mabao saba msimu huu naye amejumuishwa katika kikosi hicho. Sako sasa watakosa mechi tano za Wolves ambao wanapambana kupanda katika Ligi Kuu msimu ujao. Kiungo wa klabu ya Bordeaux Abdou Traore ni mchezaji mwingine aliyeitwa katika kikosi hicho baada ya kukosekana kwa zaidi ya mwaka mmoja. Mali ambao walimaliza katika nafasi ya tatu kwenye michuano iliyopita wamepangwa katika kundi gumu la D sambamba na timu za Ivory Coast, Cameroon na Guinea.

No comments:

Post a Comment