Monday, December 29, 2014

PARDEW AKWEPA KITIMOTO CHA WANA HABARI.

MENEJA wa klabu ya Newcastle United, Alan Pardew amekwepa kutoa kauli kuhusiana na taarifa kuwa anaweza kuwa meneja mpya wa klabu ya Crystal Palace. Pardew mwenye umri wa miaka 53, alishindwa kutimiza majukumu ya wanahabari baada ya ushindi wa mabao 3-2 waliopata dhidi ya Everton jana. Kocha msaidizi wa Newcastle John Carver ambaye ndiye aliyekwenda katika mkutano wa wanahabari amesema Pardew hakutoa sababu yeyote kwanini hakwenda kuzungumza na wanahabari hao. Palace walimtimua kocha wa Neil Warnock Jumamosi iliyopita ikiwa imepita miezi mine pekee huku timu hiyo ikiendelea kuning’inia katika mstari wa kushuka daraja.

No comments:

Post a Comment