Monday, December 29, 2014

ITACHUKUA MUDA MREFU SCHUMACHER KURUDI KATIKA HALI YAKE.

MENEJA wa dereva nyota wa zamani na bingwa wa dunia wa mashindano ya langalanga Michael Schumacher amedai kuwa bado ana safari ndefu ya kupona kutokana na majeruhi ya kichwa aliyopata katika ajali wakati akiteleza katika barafu. Meneja huyo Sabine Kehm alikaririwa akidai kuwa itachukua muda mrefu kwa Schumacher kurudi katika hali yake ya kawaida. Kauli ya Sabine imekuja baada ya taarifa kuwa Schumacher ameanza kuwasiliana na watu wake wa karibu kwa macho. Ukiwa umepita mwaka mmoja toka Schumacher apate ajali hiyo, Sebine alikanusha madai hayo kwa kudai sio taarifa za kweli.

No comments:

Post a Comment