Monday, December 29, 2014

POCHETTINO KUIONGEZEA NGUVU SPURS JANUARI.

MENEJA wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino amepanga kujadili uwezekano wa kufanya usajili wakati dirisha dogo la usajili Januari litakapofunguliwa Alhamisi hii. Spurs walimaliza mwaka 2014 kwa sare ya bila kufungana dhidi ya United katikamchezo wa Ligi Kuu uliofanyika katika Uwanja wa White Hart Lane Jana wakati wakiendelea kupambana kumaliza katika nafasi nne za juu. Timu hiyo pia imefanikiwa kutinga hatua ya timu 32 bora katika michuano ya Europa League na nusu fainali katika Kombe la Ligi katika msimu wa kwanza wa kocha huyo raia Argentina. Ili kuongeza nguvu katika kikosi chake kutokana na mashindano mengi wanayoshiriki, Pochettino amedokeza kuwa anajipanga kuleta sura mpya mwezi ujao. Pochettino amesema anafurahia kikosi alichonacho lakini kipindi cha usajili kikifika watakaa na klabu kujadili maeneo ya kuimarisha. Spurs wana kibarua kizito katika mchezo wao unaofuata dhidi ya Chelsea ambao utachezwa pia katika Uwanja wa White Hart Lane katika simu ya mwaka moja.

No comments:

Post a Comment