Monday, December 22, 2014

RONALDO ATENGENEZEWA SANAMU MAALUMU.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametengenezewa sanamu maalumu. Sanamu hilo limewekwa katika mji wa kisiwa cha Madeira nchini Ureno mahli ambapo ndipo aliposaliwa mwanasoka huyo. Ronaldo aliungana na familia yake, wakiwemo mama, kaka na dada zake kwenda kuzindua sanamu hilo. Baadhi ya wadau wa soka nchini humo wamekuwa wakiikosoa sanamu hiyo na kudai kuwa haijafanana na nyota huyo. Pamoja na sanamu, Ronaldo ana makumbusho maalum kwa ajili yake katika kisiwa cha Madeira.

No comments:

Post a Comment