Wednesday, January 28, 2015

AFCON 2015: BAADA YA GAHAN NA ALGERIA KUSONGA MBELE KUNDI C, LEO NI KUFA NA KUPONA KWA TIMU ZA KUNDI D.

TIMU kongwe za Ghana na Algeria jana zilifanikiwa kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika baada ya kushinda mechi zao za mwisho za kundi C. Ghana wenyewe walisonga mbele baada ya kutoka nyuma na kuibugiza Afrika Kusini kwa ju mla ya mabao 2-1 huku Algeria wao wakiichakaza Senegal kwa kwa mabao 2-0. Mabao ya Ghana katika mchezo huo yalifungwa na John Boye na Andre Ayew huku lile la kufutia machozi la Afrika Kusini likifungwa na Mandla Misango wakati kwa upande wa Algeria wao mabao yake yalifungwa na Riyadhi Mahrez na Nabil Bantaleb. Leo kutakuwa na mtanange mwingine wa mwisho wa makundi ambapo timu za kundi D zitakuwa uwanjani kuchuana ili kutafuta nafasi ya mbili za kwenda robo fainali zilizobakia. Katika michezo hiyo ambayo yote itachezwa kwa pamoja kuepuka upangaji matokeo wakongwe Cameroon watamenyana na Ivory Coast wengi wakifananisha mchezo huo kama fainali huku Guinea wao wakitoana jasho na Mali.

No comments:

Post a Comment