Tuesday, January 27, 2015

KINYANG'ANYIRO CHA URAIS FIFA CHAZIDI KUSHIKA KASI, RAIOLA AJITOA BAADA YA VAN PRAAG KUTANGAZA NIA.

WAKALA wa kimataifa Mino Raiola ameamua kujitoa katika mbio za kuwania urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA baada ya mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Uholanzi-KNVB Michael Van Praag kutangaza nia ya kugombea nafasi hiyo inayoshikiliwa na Sepp Blatter. Wakala huyo ambaye anawawakilisha wachezaji kama Paul Pogba, Zlatan Ibrahimovic, Mario Balotelli na Henrikh Mkhitaryan, alitangaza kugombea nafasi hiyo wiki iliyopita akidai kuwa FIFA inahitajika kubadili uongozi wake. Hata hivyo, Raiola sasa anedhani Van Praag ndio mgombea mzuri katika kinyang’anyiro hicho na kujitolea kumuunga mkono. Akihojiwa Raiola amesema kugombea urais FIFA haukua kwa ajili yake kwani ilikuwa ni kwasababu ya kupata mgombea mgombea mzuri ambaye anaweza kumpa changamoto Blatter na sasa amepatikana. Raiola amesema Van Praag ni mtu ambaye yuko vizuri kimtandao huku akiwa na subira zaidi ndio maana amefurahishwa kuachia nafasi hiyo kwa mtu kama huyo. Kujitoa kwa Raiola kunamaanisha kuwa Blatter sasa atakuwa aanapata upinzani kutoka kwa wagombea wanne akiwemo Jerome Champagne, Prince Ali Bin Al Hussein, Van Praag na David Ginola.

No comments:

Post a Comment