Tuesday, January 27, 2015

TETESI ZA USAJILI ULAYA: COSTA AGOMA KWENDA CHELSEA JANUARI HII, ALLEGRI AZIWASHIA TAA ZA KIJANI MAN UNITED NA CHESLEA KUHUSIANA NA POGBA.

KATIKA habari za tetesi za usajili, mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil Douglas Costa mwenye umri wa miaka 24 ameitaka klabu yake ya Shakhtar Donetsk kutomuuza kwenda Chelsea katika kipindi hiki cha Januari. Klabu za Manchester United na Chelsea wamepata ahueni katika mbio zao za kuwania kumsajili kiungo Paul Pogba mwenye umri wa miaka 21 baada ya meneja wa Juventus Massimiliano Allegri kudai kuwa itakuwa ngumu kukataa ofa ya paundi milioni 75 kwa ajili ya nyota huyo. Kwingineko klabu ya Man United inaweza kurudi nyuma katika mbio zao za kumsajili Kevin Strootman mwenye umri wa miaka 24 baada ya kiungo huyo wa Roma kupata majeruhi katika mchezo dhidi ya Fiorentina. Naye wakala wa winga Adnan Januzaj mwenye umri wa miaka 19 amebainisha kuwa meneja wa Man United Louis van Gaal amezuia kuondoka kwa mchezaji huyo kwenda klabu ya Paris Saint-Germain au nyingine yeyote katika kipindi hiki cha usajili wa Januari. Klabu ya Southampton inafikiria kutoa ofa kwa ajili ya kusajili kiungo wa kimataifa wa Uholanzi Jordy Clasie mwenye umri wa miaka 23 kutoka klabu ya Feyenoord. Kwa upande mwingine Andre Schurrle mwenye umri wa miaka 24 anatarajiwa kukosekana katika kikosi cha Chelsea kwenye mchezo wa maruadiano wa Kombe la Ligi dhidi ya Liverpool. Hatua hiyo inatokana na klabu ya Wolfsburg kuwa mbioni kumsajili mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani. Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anafikiria kuwasajili beki wa kulia wa Valencia Joao Pereira na beki wa kati wa AC Milan Adil Rami kabla ya kufungw akwa dirisha dogo la usajili mwezi huu.

No comments:

Post a Comment