Wednesday, January 28, 2015

BAADA YA KUTINGA FAINALI KOMBE LA LIGI, MOURINHO AMKINGIA KIFUA COSTA ADAI ALIWAKANYAGA WACHEZAJI WA LIVERPOOL KWA BAHATI MBAYA.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedai kuwa tukio la Diego Costa kuwakanyaga wachezaji wa Liverpool katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Ligi, kilikuwa cha bahati mbaya. Katika mchezo huo war obo fainali Chelsea walishinda kwa bao pekee lililofungwa na Branislov Ivanovic mwanzoni mwa dakika za nyongeza baada ya timu hizo kutoka sare ya bila kufungana katika muda wa kawaida. Costa aliwakanyaga Emre Can na Martin Skrel katika mchezo huo wa mkondo wa pili uliofanyika katika Uwanja wa Stamford Bridge. Mourinho amesema wakati mchezaji wa upinzani akiwa amelala chini, Costa alimkanyaga kwa bahati mbaya wakati akiwajaribu kuchukua mpira. Hata hivyo kauli hiyo inapingwa vikali na meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers ambaye amesema kwa ushahidi wa picha za video inaonyesha wazi kabisa kuwa Costa aliwakanyaga wachezaji hao kwa makusudi. Chelsea sasa wanasubiria mshindi kati ya Sheffield United na Tottenham Hotspurs kwa ajili ya kucheza naye fainali itakayofanyika machi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment