Wednesday, January 28, 2015

ASIA CUP 2015: AUSTRALIA KUKWAANA NA KOREA KUSINI FAINALI.

NAHODHA wa timu ya taifa ya Australia, Tim Cahill anatarajiwa kuingoza timu hiyo katika mchezo wa fainali wa Kombe la Asia dhidi ya Korea Kusini utakaochezwa Jumamosi hii. Cahill ambaye katika kipindi cha maiak 17 ya usakataji kabumbu hajawahi kushinda taji lolote kubwa, hii itakuwa nafasi pekee ya kufanya hivyo kabla ya kustaafu soka. Mbele ya mashabiki 80,000 watakaohudhuria fainali hiyo itakayofanyika jiji Sydney, Cahill ataingoza Australia mbele ya mashabiki wa nyumbani kupambana na timu hiyo ngumu ya Korea Kusini. Akihojiwa mara baada ya kuitandika Umoja wa Falme za Kiarabu-UAE kwa mabao 2-0 katika mchezo nusu fainali, Cahill aliwashukuru wachezaji wenzake, viongozi na mashabiki wote waliokuwa wakiwaunga mkono kuanzia mwanzo. Cahill amesema ilikuwa ni safari ndefu lakini sasa wana kibarua kimoja cha kuzingatia mechi kubwa katika historia ya soka la Australia.

No comments:

Post a Comment