Wednesday, January 28, 2015

ARSENAL YAMPELEKA CAMPBELL KWA MKOPO VILLARREAL ILI WAMCHUKUE PAULISTA.

MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Joel Campbell amejiunga na klabu ya Villarreal kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu. Uhamisho wa nyota huyo wa kimataifa wa Costa Rica kwenda Hispania ni sehemu ya mpango ambao Arsenal wanajipanga kumsajili beki wa Villarreal Gabriel Paulista ambaye tayari ameshafaulu vipimo vya afya katika klabu hiyo ya London kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza. Campbell alituma ujumbe katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter ukiwa sambamba na picha yake akiwa amevaa skafu ya Villarreal akiwashukuru wanafamilia wa Arsenal kwa ujumbe wao wa kumtakia heri na kuahidi kuwaletea sifa. Paulista mwenye umri wa miaka 24 anatarajiwa kuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Arsenal katika kipindi hiki cha Januari baada ya kusajiliwa kwa mchezaji kinda kutoka Poland Krystian Bielik.

No comments:

Post a Comment