Wednesday, January 21, 2015

ASTON VILLA YAMKOMALIA BENTEKE.

MENEJA wa klabu ya Aston Villa, Paul Lambert amedai kuwa hawatakubali ofa yeyote kwa mshambuliaji wao Christian Benteke ili waweze kuimarisha safu yao ya ushambuliaji. Villa wako katika nafasi ya 15 katika msimamo wa Ligi Kuu, wakiwa alama tatu juu ya mstari wa kushka daraja huku wakiwa wamefunga mabao 11 katika mechi 22 walizocheza. Kutoka hali ilivyo Lambert amesema hawezi kukubali kumuuza Benteke katika kipindi cha usajili wa Januari kwnai wanahitaji nguvu ili waweze kupambana na balaa la kushuka daraja. Lambert aliendelea kudai kuwa hana shaka kwamba mmliki wa Villa Randy Lerner atauelewa uamuzi wake huo kwa manufaa ya klabu. Benteke amefunga mabao mawili katika mechi 13 za Ligi Kuu alizocheza msimu huu.

No comments:

Post a Comment