Tuesday, January 27, 2015

RODRIGUEZ AMKINGIA KIFUA RONALDO.

KIUNGO mahiri wa Real Madrid, James Rodriguez amedai kumhusudu Cristiano Ronaldo na kupuuza taarifa kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ureno ni mkorofi. Rodriguez alijiunga na Madrid akitokea Monaco kwa kitita cha euro milioni 80 mwanzoni mwa msimu huu na amekuwa akivutiwa na maadili ya kazi aliyonayo Ronaldo. Akihojiwa Rodriguez amesema Ronaldo ni mchezaji mwenye tabia nzuri ndani na nje ya uwanja na kwake anadhani ndio alistahili tuzo ya Ballon d’Or aliyopata kwa mafanikio aliyopata mwaka 2014. Rodriguez aliendelea kudai kuwa wamekuwa na mahusiana mazuri na nyota huyo na amekuwa akimvutia kwa jinsi anavyojituma mazoezini.

No comments:

Post a Comment