Thursday, January 22, 2015

RONALDO AZIKATA MAINI MAN UNITED NA CHELSEA KWA KUDAI HANA MPANGO WA KWENDA UINGEREZA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo amewanyong’onyesha mashabiki wa klabu za Manchester United na Chelsea baada ya kudai kuwa amepanga kwenda kumalizia soka lake nchini Brazil mara baada ya kuondoka Hispania. Wadau wengi walikuwa akitabiri kuwa Ronaldo anaweza kurejea United mara baada ya kumaliza mkataba wake Madrid lakini mwenyewe amekaririwa na gazeti la Metro akidai kutimkia Brazil katika klabu za Corinthians au Flamengo. Ronaldo ambaye ameitumikia United kwa muda wa miaka sita kabla ya kuhamia Madrid mwaka 2009 amekuwa akieleza mapenzi yake kwa mashabiki wa timu hiyo huku akihusihwa pia na kwenda Chelsea. Ronaldo alikaririwa akidai kuwa Corinthians na Flamengo ni vilabu vikubwa ambavyo anaweza kucheza katika mojawapo kwani amekuwa na marafiki wengi sana Brazil.

No comments:

Post a Comment