Thursday, February 19, 2015

ALIYEBAGULIWA NA MASHABIKI WA CHELSEA JIJINI PARIS ATAKA KUCHUKULIWA HATUA.

MTU aliyekuwa akizuiwa kuingia katika treni jijini Paris na mashabiki wa soka wa Chelsea waliokuwa wakiimba nyimbo za kibaguzi, ametaka wote waliohusika kuchukuliwa hatua. Mtu huyo aliyejulikana kwa jina la Souleymane S, mwenye umri wa miaka 33 alikaririwa na gazeti moja nchini Ufaransa akidai watu hao ambao ni mashabiki wa Uingereza wanapaswa kuwekwa lupango. Katika picha za video ziliomuonyesha Souleymane akiingia katika treni lakini alisukumwa na mashabiki hao waliokuwa wakiimba nyimbo kuwa wao ni wabaguzi. Kitendo hicho kimekemewa vikali na watu mbalimbali ikiwemo klabu ya Chelsea ambayo msemaji wake ametaka hatua stahiki kuchukuliwa kwa wale wote waliohusika.

No comments:

Post a Comment