Friday, February 20, 2015

GERRARD AMPASHA BALOTELLI KWA KUKOSA HESHIMA.

KIUNGO wa Liverpool, Steven Gerrard amemtuhumu Mario Balotelli kwa kukosa heshima kutokana na kuchukua jukumu la kupiga penati badala ya Jordan Henderson katika mchezo dhidi ya Besiktas. Balotelli alifunga penati hiyo kwenye mchezo wa michuano ya Europa League hatua ya 32 bora na kuifanya Liverpool kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0. Hatua ya Balotelli imekuja kufuatia nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel Sturridge kutokubaliana juu ya nani haswa anayestahili kupiga mkwaju huo wa penati. Akihojiwa Gerrard amesema Henderson ndiye aliyekuwa nahodha na Balotelli alionyesha utovu wa nidhamu kidogo. Katika mchezo huo Gerrard alikuwa nje kutokana na na kusumbuliwa na majeruhi.

No comments:

Post a Comment