Friday, February 20, 2015

CHELSEA YASIMAMISHA WATATU KUHUSIANA UBAGUZI PARIS.

KLABU ya Chelsea imewasimamisha watu watatu kuhudhuria katika Uwanja wake wa Stamford Bridge baada ya kutolewa kwa picha za video zikiwaonyesha mashabiki wa timu hiyo wakimzuia mtu mwenye asili ya Afrika kuingia katika treni jijini Paris. Klabu hiyo imedai kuwa adhabu ya kufungiwa maisha inaweza kuwakabili mashabiki hao kama wakikutwa na hatia ya kujihusisha na kitendo. Picha za video zilionyesha mtu huyo akisukumwa kutoka katika treni wakati kundi la mashabiki likiimba nyimbo za kibaguzi. Polisi wanalifanyia uchunguzi tukio hilo lililotokea kabla ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Chelsea na Paris saint-Germain ambao ulimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1 Jumanne iliyopita.

No comments:

Post a Comment