Friday, February 20, 2015

TUNISIA YAKATA RUFANI CAS.

TUNISIA nayo imekata rufani Mahakama ya Kimataifa ya Michezo-CAS jana kufuatia utata uliojitokeza katika michuano ya Mataifa ya Afrika yaliyomalizika mapema mwezi huu. Tunisia ambao walichapwa kwa mabao 2-1 na wenyeji Guinea ya Ikweta katika hatua ya robo fainali, wamekata rufani kupinga amri ya kuwataka kuomba radhi kwa kulituhumu Shirikisho la Soka la Afrika-CAF kwa upendeleo. Tunisia iliamriwa na CAF kuwa watatolewa katika mashindani ya kufuzu michuano hiyo katika michuano ijayo ya Afcon mwaka 2017 kama hawatatimiza amri hiyo mpaka mwishoni mwezi ujao. Tunisia walikuja juu baada ya wenyeji Guinea ya ikweta kuzawadiwa penati katika dakika za majeruhi ambayo iliwafanya kusawazisha bao kabla ya kushinda kwa mabao 2-1 katika muda wa nyongeza. Picha za video ziliwaonyesha wachezaji wa Tunisia wakimkimbiza mwmauzi na kujaribu kumpiga mwishoni mwa mchezo huo.

No comments:

Post a Comment