Friday, February 20, 2015

MODRIC AANZA KUFANYA MAZOEZI.

KIUNGO wa Real Madrid Luka Modric ameanza kufanya mazoezi na wenzake kwa mara ya kwanza jana baada ya kupita kipindi cha miezi mitatu ikiwa ni ishara za kukaribia kurejea uwanjani baada ya kupona majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua. Klabu hiyo ilithibitisha nyota huyo wa kimataifa wa Croatia kufanya mazoezi sambamba na wachezaji ambao hawakuanza katika mchezo wa Ligi ya mabingwa Ulaya ambao Madrid ilishinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Schalke Jumatano. Modric alipata majeruhi wakati akiitumikia timu yake ya taifa katika mechi ya kufuzu michuano ya Ulaya mwaka 2016 dhidi ya Italia Novemba mwaka jana. Nyota huyo wa zamani wa Tottenham Hotspurs amekosa mechi 21 zilizopita za Madrid ikiwamo michuano ya Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia iliyofanyika Desemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment