Friday, February 20, 2015

FIGO ATAKA MDAHALO NA BLATTER.

MGOMBEA urais wa Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA, Luis Figo ana matumaini ya kumpa shinikizo rais wa sasa Sepp Blatter kwa kutaka kufanyika mdahalo wa wazi kabla ya uchaguzi miongoni mwa wagombea wote wanne. Prince Ali bin Al Hussein alitoa wazo hilo wakati akifungua kampeni zake kwa ajili ya kugombea nafasi hiyo mapema mwezi huu na wakati Figo akiulizwa kama amejiandaa na hilo akadai hana shaka. Figo amesema anaamini katika mawazo yake kwani kama yakifanyiwa kazi hakuna shaka kwamba yatabadilisha mfumo mzima wa shirikisho hilo kwa ajili ya faida ya siku zijazo. Winga huyo wa zamani wa kimataifa wa Ureno na klabu za Barcelona na Real Madrid mwenye umri wa miaka 42 anatarajiwa kuchuana na Blatter, Prince Ali rais wa Shirikisho la Soka la Asia na Jordan na rais wa Shirikisho la Soka la Uholanzi Michael van Praag katika kinyang’anyiro hicho kitakachofanyika Mei 29 mwaka huu jijini Zurich.

No comments:

Post a Comment