Friday, February 20, 2015

MASHABIKI 23 WA FEYENOORD WAKAMATWA JIJINI ROME.

MASHABIKI 23 wa klabu ya Feyenoord wamekamatwa jijini Rome na 19 kati yao wakishitakiwa baada ya kufanyika vurugu kabla ya mchezo wa michuano ya Europa League dhidi ya AS Roma jana na kusababisha hasara katika mji huo. Mashabiki waliokuwa wamelewa waliharibu baadhi ya majengo na kuwarushia chupa polisi Jumatano usiku kabla ya mamia wengine kugombana na polisi jana kabla ya kuanza kwa mchezo huo. Polisi walilazimika kufyatua mabomu ya machozi na kuwatawanya mashabiki hao ambao waliacha eneo hilo likiwa limejaa chupa tupu za bia. Kwa mujibu wa maofisa wa polisi wa Rome mashabiki wengi wameshitakiwa kwa kosa la kukataa kukamatwa na kuongeza kuwa wanaweza kukabiliwa kifungo cha miezi sita au faini ya euro 45,000. Mashabiki wapatao 6,500 walisafiri kwenda jiji Rome kwa ajili ya kushuhudia mchezo huo wa mkondo wa kwanza ambao Feyenoord walifanikiwa kupata sare ya bao 1-1.

No comments:

Post a Comment