Friday, February 20, 2015

IBRAHIMOVIC ALIMWA ADHABU MECHI MBILI.

LIGI Kuu nchini Ufaransa-LFP imetangaza jana kumfungia mechi mbili mshambuliaji nyota wa Paris Saint-Germain-PSG, Zlatan Ibrahimovic. Nyota huyo wa kimataifa wa Sweden alilimwa adhabu hiyo katika kikao cha kamati ya nidhamu ya ligi kilichokutana kufuatia tukio lake na Romain Hamouma katika ushindi wa bao 1-0 waliopata PSG dhidi ya Saint-Etienne mwezi uliopita. Ibrahimovic sasa atakosa mchezo dhidi ya Monaco utakaochezwa Jumapili hii na mchezo mwingine war obo fainali ya Kombe la Ligi utakaochezwa Jumatano ijayo na timu hiyohiyo. Nyota huyo ameshafunga mabao 17 katika mshindano yote msimu huu akiwa sambamba na Edinsoni Cavani.

No comments:

Post a Comment