Friday, February 20, 2015

MARTINEZ AMMWAGIA SIFA LUKAKU BAADA YA KUPIGA HAT-TRICK.

MENEJA wa klabu ya Everton Roberto Martinez amesema mshambuliaji Romelu Lukaku ameonyesha kujitoa kutokana na kiwango chake katika mchezo wa jana ambao walishinda mabao 4-1 dhidi ya Young Boys. Katika mchezo huo Lukaku alifunga hat-trick yake ya kwanza akiwa na klabu hiyo na kuipa uahindi muhimu katka mchezo wao wa mkondo wa kwanza wa michuano ya Europa League. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 21 aliwakera mashabiki wa timu hiyo mapema mwezi huu kwa kukaririwa na gezeti moja akiwa kuwa na matumaini ya kuondoka kwenda katika klabu kubwa. Hata hivyo, Martinez alimtetea Lukaku na kudai kuwa anapenda kuitumikia Everton na hilo ameonyesha jana kwa kiwango bora alichoonyesha.

No comments:

Post a Comment