Friday, February 20, 2015

BONY ATAMBA KUISAIDIA CITY KUTETEA TAJI LA LIGI KUU.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ivory Coast, Wilfried Bony anaamini anaweza kuwa silaha ya siri kwa Manchester City katika mbio zao za ubingwa wa Ligi Kuu wakati akijiandaa kucheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Newcastle United Jumamosi hii. Bony alijiunga na City inayonolewa na Manuel Pellegrini akitokea Swansea City kwa kitita cha paundi milioni 28 Januari mwaka huu lakini bado hajacheza mechi yeyote kutokana na majukumu ya kimataifa aliyokuwa nayo katika michuano ya Mataifa ya Afrika. Sasa nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 atapata nafasi kwa mara ya kwanza kuwaonyesha mashabiki wa City na kuwapa matumaini mapya ya kutetea taji lao. Bony ambaye alifunga mabao 34 katika mechi 70 alizoichezea Swansea ana uhakika kuwa anaweza kuisaidia timu hiyo kufikia malengo yake. City wanashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi wakiwa nyuma ya vinara ya Chelsea.

No comments:

Post a Comment