Friday, February 20, 2015

TETESI ZA USAJILI UALAYA: VAN GAAL KUTUMIA EURO MILIONI 200 KATIKA USAJILI KIANGAZI, CHELSEA KUMPA MOURINHO MIAKA MINGINE MINNE.

KATIKA habari za tetesi za usajili zilizopamba vichwa habari katika mitandao mbalimbali barani Ulaya ni pamoja na meneja wa Manchester United Louis van Gaal ametaja majina ya wachezaji anaoweza kuwasajili katika majira kiangazi huku akiwa tayari kutumia kitita cha euro milioni 200. Van Gaal amewataja wachezaji anaowawinda ambao ni Nathaniel Clyne, Mats Hummels, Kevin Strootman, Memphis Depay na Paulo Dybala. Meneja wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho anatarajiwa kusaini mkataba mpya na timu hiyo katika majira ya kiangazi. Kocha huyo raia wa Ureno kwasasa anafurahia kuwepo Stamford Bridge na anataka kuendelea kubakia hapo huku klabu hiyo ikitegemea kumsainisha mkataba wa miaka minne. Klabu ya Arsenal imepata upinzani katika mbio zao za kutaka kumsajili Lars Benders baada ya Barcelona kuonyesha nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo wa Bayer Leverkusen. Barcelona wameamua kumuweka Bender katika mipango yao ya usajili huku Arsenal wakihamishia nguvu zao kwa Morgan Schneiderlin. Manchester United wamejitoa katika mbio za kutaka kumsajili Paulo Pogba katika majira ya kiangazi. Meneja wa United Louis van Gaal anamhusudu kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa lakini klabu haiku tayari kumnunua tena mchezaji huyo ambaye walimruhusu kuondoka kama mchezaji huru kwenda Juventus. Chelsea wameipiga bao Arsenal katika kinyang’anyiro cha kutaka kumsajili nyota wa Palermo Paulo Dybala. Arsenal walifanya mazungumzo na klabu hiyo ya Italia lakini Jose Mourinho sasa ndio anaongoza mbio hizo kwa kuwa tayari kutoa kitita cha euro milioni 40 kwa ajili ya mshambuliaji huyo ili aweze kuziba nafasi ya Drogba.

No comments:

Post a Comment