Monday, February 23, 2015

CHELSEA KUKATIA RUFANI KADI NYEKUNDU YA MATIC.

KLABU ya Chelsea inajipanga kukata rufani dhidi ya kadi nyekundu aliyopewa Nemanja Matic wakati wa mchezo wao dhidi ya Burnley ambao ulimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1 Jumamosi uliyopita. Kiungo huyo wa kimataifa wa Serbia mwenye umri wa miaka 26 alitolewa kwa kumsukuma Ashley Barnes mpaka kuanguka baada ya kugongana wakigombea mpira. Chelsea ambao ndio vinara wa Ligi Kuu wamepewa mpaka kesho wawe wamewasilisha ushahidi wao Chama cha Soka cha Uingereza-FA. Kama rufani yao ikikataliwa Matic anatarajiwa kukosa mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi utakaofanyika Jumapili hii dhidi ya Tottenham Hotspurs.

No comments:

Post a Comment