Monday, February 23, 2015

ANCELOTTI AKIRI KUSHANGAZWA NA KICHAPO CHA BARCELONA.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amekiri kuwa alishtushwa na kipigo cha bao 1-0 walichopata Barcelona dhidi ya Malaga lakini bado anategemea mbio za ubingwa wa La Liga kuendelea mpaka siku ya mwisho. Barcelona walikuwa wakitawala kwa kushinda mechi 11 mfululizo katika mashindano yote kabla ya rekodi hiyo kutibuliwa na Malaga katika Uwanja wa Camp Nou Jumapili iliyopita. Akihojiwa mara baada ya Madrid kuichapa Elche mabao 2-0, Ancelotti amesema mchezo huo ulikuwa muhimu hususani baada ya mahasimu wao Barcelona kuteleza. Ancelotti aliendelea kudai kuwa ni wazi kipigo hicho kiliwashangaza watu wote kutokana na kiwango bora walichonacho sasa.

No comments:

Post a Comment