Monday, February 23, 2015

RANALDO APAA MPAKA NAFASI YA TATU KATIKA ORODHA YA WAFUNGAJI BORA MADRID, ABAKISHA MABAO 33 AFIKIE REKODI YA RAUL.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amepaa mpaka nafasi ya ya tatu katika orodha ya wafungaji bora wa klabu hiyo baada ya kufunga bao katika mchezo dhidi ya Elche uliochezwa jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alifunga bao lake la 290 toka aanze kuitumikia Madrid na kupanda juu ya nguli wa zamani wa klabu hiyo Carlos Santillana na sasa amebakisha mabao 33 kumfikia nyota wa zamani Raul mwenye mabao 323. Katika mchezo huo Karim Benzema aliifungia Madrid bao la kuongoza kabla ya Ronaldo hajafunga bao la pili katika kipindi cha pili na kuifanya timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-0. Madrid bado wanaendelea kushikilia usukani wa La Liga kwa tofauti ya alama nne dhidi ya mahasimu wao Barcelona.

No comments:

Post a Comment