Monday, February 23, 2015

AOMBA RADHI KUFUATIA SAKATA LA TUHUMA ZA UBAGUZI LA MASHABIKI WA CHELSEA.

OFISA wa zamani wa polisi na mshabiki wa Chelsea ameomba radhi kwa kuhusika na tuhuma za tukio la ubaguzi katika kituo cha treni jijini Paris lakini amedai yeye sio mbaguzi. Richard Barklie mwenye umri wa miaka 50 alitambuliwa kama mmoja wa watu ambao wanafanyiwa uchunguzi na polisi. Katika taarifa yake, Barklie alikanusha kuimba nyimbo za kibaguzi na kudai kuwa alikuwa akitaka kufafanua kwa polisi jinsi tukio hilo lililovyokuwa. Chelsea imeshawasimamisha mashabiki watano baada ya picha za video kuonyesha mtu mwenye asili ya kiafrika akizuiwa kuingia katika treni.

No comments:

Post a Comment