Monday, February 23, 2015

KOMPANY ATAMBA KUWA HAWAIOGOPI CITY.

NAHODHA wa klabu ya Manchester City, Vincent Kompany amesema kikosi chao hakiwaogopi Barcelona ambao wanakutana nao katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya mtoano. Barcelona iliwang’oa City kwa kuwachapa kwa jumla ya mabao 4-1 katika hatua kama hiyo msimu uliopita. Mchezo wa mkondo wa kwanza baina ya timu hizo utafanyika katika Uwanja wa Etihad kesho kabla ya kurudiana tena Machi 18 katika Uwanja wa Camp Nou. Akihojiwa Kompany amesema hawana hofu yeyote na Barcelona na wana uhakika wanaweza kuwang’oa kutokana na kiwango bora walichonacho.

No comments:

Post a Comment