Tuesday, February 24, 2015

ENRIQUE AMKINGIA KIFUA MESSI PAMOJA NA KUKOSA PENATI.

MENEJA wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique amesisitiza kuwa Lionel Messi ataendelea kuwa mpiga penati wa timu hiyo pamoja na kukosa penati yake ya tatu msimu huu katika mchezo dhidi ya Manchester City jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alikuwa na nafasi ya kuipa ushindi Barcelona wa mabao 3-1 katika dakika za majeruhi lakini Joe Hart alifanikiwa kuokoa mchomo wake. Messi pia amekosa penati katika mchezo dhidi ya Levante Septemba mwaka jana na Brazil wakati akiitumikia timu yake ya taifa Octoba lakini Enrique anaamini kuwa nyota huyo bado ni mpigaji mzuri na anamuamini. Kocha huyo amesema wale wote wanaokosa penati ni wale wenye uthubutu wa kufanya hivyo na Messi bado ataendelea kuwa mpigani wao. Katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza uliofanyika katika Uwanja wa Etihad, Barcelona ilifanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment