Thursday, February 19, 2015

ANCELOTTI ADAI RONALDO AMEREJESHA MAKALI YAKE.

MENEJA wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amesema Cristiano Ronaldo amerejea katika makali yake baada ya nyota huyo kumaliza ukame wa mabao katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Schalke jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno amekuwa katika kipindi kigumu kidogo katika wiki za karibuni akiwa amekosa mechi mbili za La Liga akitumikia adhabu huku akiwa hajafunga bao toka Januari 18 mwaka huu. Hata hivyo bao la kichwa alilofunga katika kipindi ca kwanza katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya mtoano uliwaziba mdomo wale wote waliokuwa wakihoji uwezo wake. Sasa Ronaldo anakuwa amekuwa Lionel Messi na Raul kwa kufikisha mabao 76 katika michuano hiyo. Akihojiwa Ancelotti amesema anafurahi kwani Ronaldo amerejea katika kiwango chake kutokana na alivyocheza vyema katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment