Thursday, February 19, 2015

VAN GAAL AONYWA KWA KAULI YAKE.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Louis van Gaal ameonywa kwa siku zijazo kuhusiana na kauli yake aliyotoa baada ya mchezo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana na Cambridge United katika mchezo wa Kombe la FA mwezi uliopita. Mara baada ya mchezo huo Van Gaal aliiambia BBC kuwa kila kitu kilikuwa tofauti na kikosi chake aikiwemo na mwmauzi wa mchezo. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kiliamua kuw akauli hiyo ilikuwa sheria lakini kocha huyo aliepuka faini na kupewa onyo. United sasa itachuana na Arsenal katika Uwanja wa Old Trafford kwenye mchezo wa robo fainali ya michuano hiyo ambapo Van Gaal atakuwa akitafuta ushindi ili aweze kunyakuwa taji lake la kwanza katika msimu wa kwanza akiwa kocha.

No comments:

Post a Comment