Thursday, February 19, 2015

KOCHA WA PORTO ALALAMIKIA MATOKEO WALIYOPATA.

MENEJA wa klabu ya FC Porto Julen Lopetegui amesisitiza kuwa kikosi chake kilikuwa imara zaidi katika mchezo dhidi ya FC Basel kuliko zilivyokuwa Real Madrid na Liverpool mwanzoni mwa msimu, hivyo hadhani kama walistahili sare ya bao 1-1 waliyopata. Wenyeji Basel ndio waliotangulia kufunga bao kupitia kwa Derlis Gonzalez katika dakika ya 11 na kuwafanya Porto kuwa nyuma kwa kipindi kirefu cha mchezo huo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora kabla ya Danilo kuisawazishia bao kwa penati dakika 79. Akihojiwa na wanahabari mara baada ya mchezo huo kocha huyo amesema hatua ya mtoano katika michuano hiyo huwa inachanganya hivyo walikuwa wako tayari kupambana na magumu yeyote. Lopetegui amesema wapinzani wao Basel walifunga bao kwa shuti moja lililolenga lango lakini wao walipiga mengi lakini wakaambulia goli moja lakini anadhani walistahili matokeo zaidi ya hayo.

No comments:

Post a Comment