Thursday, February 19, 2015

HATIMAYE WEST HAM WAMNASA NENE.

KLABU ya West Ham United imefanikiwa kumnasa winga wa kimataifa wa Brazil Nene kwa mkataba wa muda mfupi. West Ham ililazimika kuchukua hatua hiyo haraka ili kuziba nafasi ya Andy Carroll ambaye hatacheza kw amsimu wote uliobakia kutokana na majeruhi ya goti. Nene mwenye umri wa miaka 33 alikuwa akizichezea klabu za Ligi Kuu Ufaransa Monaco na Paris Saint-Germain kabla ya kujiunga na klabu ya Al-Gharafa ya Qatar mwaka 2013. Akihojiwa Nene amesema anajivunia kwenda katika klabu kubwa kama West Ham kwani alikuwa akifikiria kwa miezi kadhaa kurejea katika soka la Ulaya kutokana na ushindani uliopo.

No comments:

Post a Comment