Thursday, February 19, 2015

KOMBE LA DUNIA MWAKA NCHINI QATAR KUFANYIKA NOVEMBA NA DESEMBA MWAKA 2022.

MTANDAO mmoja barani Ulaya umetoa taarifa kuwa tayari muafaka umeshafikiwa kwa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar mwaka 2022 kufanyika katika kipindi cha Novemba na Desemba ili kuwepa joto kali katika kipindi cha kiangazi. Wakiorodhesha vyanzo mbalimbali mtandao huo umedai kuwa uamuzi umeshafanyika kwani kikosi kazi kilichoteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kinatarajia kuwasilisha miezi hiyo katika kikao chao kitakachofanyika wiki ijayo jijini Doha kabla ya kamati ya utendaji haijakamilisha mpango huo wakati wa kikao cha mwezi ujao jijini Zurich. Wiki tatu zilizopita, katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke katika mahoajiano yake na radio moja nchini Ufaransa alisema Kombe la Dunia nchini Qatar linatakiwa kuandaliwa wakati wa majira ya baridi lakini kugongana na michuano ya olimpiki ya kwenye baridi Februari mwaka 2022 pia ni hatihati. Hata hivyo mpango huo haujafafanua kwa undani zaidi kuwa michuano ya Kombe la Shirikisho ambayo huchezwa mwaka mmoja kabla ya Kombe la Dunia kama nayo itasogezwa mbele kuepuka majira ya kiangazi. Desemba mwaka jana Chama cha Vilabu barani Ulaya na Muungano wa Ligi za Soka barani humo vilipendekeza michuano hiyo ya Qatar kuchezwa kati ya May na Juni ili kutovuruga ratiba zingine za kawaida za msimu.

No comments:

Post a Comment