Wednesday, February 25, 2015

CHAMPIONS LEAGUE: BIG MATCH ARSENAL VS MONACO.

MICHUANO ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya timu 16 bora mechi za mkondo wa kwanza inaendelea tena leo ambapo katika michezo ya leo Arsenal watakuwa nyumbani kuwakaribisha Monaco huku Atletico Madrid wao wakiwa wenyeji wa Bayer Leverkusen. Arsenal watakuwa wakikwaana na Monaco kwa mara ya kwanza katika hatua hiyo lakini kwa meneja Arsene Wenger, Monaco hawatakuwa wageni kwake. Wenger amewahi kuinoa Monaco kwa miaka saba kuanzia mwaka 1987 mpaka 1994 kabla ya kuondoka na kwenda kuifundisha klabu ya Nagoya Grampus ya Japan. Huu utakuwa mchezo wa kwanza rasmi kwa Wenger dhidi ya timu yake hiyo ya zamani ambao wametinga hatua hiyo ya mtoano kwa mara ya kwanza baada ya kupita muongo mmoja. Monaco walitinga hatua hiyo wakiwa washindi wa kundi C, ingawa alama zao 11 walizopata hazikufikia zile za Arsenal ambao walimaliza katika nafasi ya pili katika kundi D nyuma ya Borrusia Dortmund. Pamoja na kutokutana katika mechi za mashindano lakini Monaco imewahi kucheza na Arsenal katika mchezo wa kirafiki Agosti 3 mwaka jana wakati wa maandalizi ya msimu mpya ambapo Monaco walishinda kwa bao 1-0 lilifungwa na Radamel Falcao kabla hajatimkia Manchester United.

No comments:

Post a Comment