Wednesday, February 25, 2015

FIFA YADAI HAKUNA KLABU ITAKAYOLIPWA KWA KOMBE LA DUNIA KUHAMISHWA.

SHIRIKISHO la Soka la Dunia-FIFA limetunisha misuli yake tena leo wakati walipotangaza kuwa hawatarajii kufidia klabu yeyote kwa kuwakosa wachezaji wao na kuleta mkanganyiko katika ligi kutokana na michuano ya Kombe la Dunia nchini Qatar kuandaliwa majira ya baridi. Siku moja baada ya kikosi kazi cha FIFA kutoa mapendekezo ya michuano hiyo kufanyika Novemba na Desemba, Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Jerome Valcke amewaambia wana habari kuwa hakuta kuwa na malipo yeyote ya kifedha kwa usumbufu utakaojitokeza katika ligi. Valcke amesema hawatalipa fidia kwasababu ligi zote zina miaka saba mpaka kufikia muda wa mashindano kupanga mikakati yao kuhakikisha michuanpo hiyo haileti mvurugano katika ligi zao. Tarehe halisi ya kuchezwa michuano hiyo inatarajiwa kupangwa na FIFA katika kikao chake cha kamati ya utendaji mwezi ujao huku kukiwa na uwezekano wa timu kupungua kutoka 32 hadi 28 kutokana na muda watakaokuwa nao.

No comments:

Post a Comment