Wednesday, February 25, 2015

PELLEGRINI ADAI ALITUMIA MBINU SAHIHI KATIKA MCHEZO DHIDI YA BARCELONA.

MENEJA wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini amesisitiza hajutii mbinu alizotumia katika mchezo wao dhidi ya Barcelona ambao wamechapwa mabao 2-1 katika Uwanja wa Etihad jana. Katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, City walitumia mfumo wa 4-4-2 lakini walijikuta wakishindwa kuhimili vishindo vya Barcelona baada ya Luis Suarez kufunga mabao mawili katika kipindi cha kwanza. Mabingwa hao wa Ligi Kuu sasa wanakabiliwa kibarua kizito katika mchezo wao wa marudiano ambao utachezwa baada ya wiki mbili katika Uwanja wa Camp Nou. Akihojiwa Pellegrini amesema amefurahi kwani ndio jinsi walivyotakiwa kucheza dhidi ya timu kama Barcelona. Kocha huyo aliongeza kuwa walicheza kwa mifumo miwili tofauti katika kipindi cha kwanza na cha pili kwani kwani kabla ya kufungwa bao la kwanza ulikuwa ni mchezo wa kawaida lakini baada ya kufungwa hali ikabadilika na wakaanza kuchezwa hovyo. Hata hivyo, Pellegrini anashukuru kwani katika kipindi cha pili wachezaji wake walibadilika na kuja kupata bao moja ambalo litakuwa muhimu kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano.

No comments:

Post a Comment