Wednesday, February 25, 2015

CHELSEA WALALAMA PAMOJA NA MATIC KUPUNGUZIWA ADHABU.

KIUNGO wa klabu ya Chelsea Nemanja Matic amepunguziwa adhabu yake kutoka mechi tatu mpaka mbili lakini bado anatarajiwa kukosa mchezo fainali ya Kombe la Ligi Jumapili hii. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kiliamua kupunguza adhabu hiyo baada ya kuridhishwa na utetezi uliotolewa na Chelsea. Matic mwenye umri wa miaka 26 alitolewa nje Jumamosi iliyopita wakati Chelsea walipotoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Burnley baada ya kumchezea vibaya Ashley Barnes. Katika taarifa yake, klabu hiyo imedai kushtushwa na kusikitishwa kuwa Matic bado atatakiwa kutumikia adhabu. Matic sasa atakosa mchezo wa fainali wa Kombe la Ligi dhidi ya Tottenham Hotspurs ambao utafanyika katika Uwanja wa Wembley na mchezo mwingine dhidi ya West Ham United Machi 4 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment