Thursday, February 26, 2015

WENGER ALIA NA SAFU YAKE YA ULINZI BAADA YA KIPIGO.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ameiponda safu yake ya ulinzi baada ya timu hiyo kuchapwa mabao 3-1 nyumbani na Monaco jana. Mabao yaliyofungwa na Geoffrey Kondogbia, Dimitar Barbatov na Yannick Ferreira-Carrasco yalitosha kuipa ushindi Monaco hivyo kuwaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Mara baada ya mchezo huo Wenger amekiri kikosi chake hakikujilinda vyema huku akiwapongeza wapinzani wao kwa kujipanga vyema. Wenger amesema ulikuwa usiku mbaya kwao lakini anawapongeza Monaco kwa kupambana, kujilinda vizuri na kutumia vyema mipira ya kushtukiza waliyopata.

No comments:

Post a Comment